Sunday, 26 June 2016

ADABU:MAKRUHU YA KUACHA KUENDELEA KUSOMA QUR'AN KWA AJILI YA MAMBO MENGINE

Yampasa kila msomaji wa qur'an kutoacha kuendelea kusoma qur'an ila kwa jambo la umuhimu si vizuri mtu kukatisha kuacha kusoma qur'an kwa ajili ya mambo yake ya kidunia,kwa masikitiko makubwa wengi wetu waislamu utamuona mtu yupo msikitini kisha huanza kuangalia huku na huku kwa ajili ya kuangalia nani anaingia msikitini kwani tabia kama hiyo hutokana na Sheitwan ambaye hamtakii mema muislam.Imesimuliwa na mmoja kati ya matabii,Naafai amesimulia kwamba Ibn Umar alikuwa aongea neno lingine lolote mpaka amalizapo kusoma Quraan" pia Naafai anaendelea kusema kwamba alikuwa na Ibn umar siku moja alisoma surat Baqara kisha akasimama na akamuuliza unajua hii imeshuka kwa mnasaba gani akamwambia sifahamu,kisha akamuelekeza hii ni kwa sababu fulani na fulani hiyo ni namna Ibn umar alivyo ishi alikua akati usomaji wake wa quraan isipokuwa kwa ajili ya kutoa elimu ambayo ni moja kati ya Ibada.

No comments :